Thursday 9 October 2014

maji katika mwili mwil wa binadamu


Umuhimu wa maji katika mwii wa binadamu

Maji ni muhimu sana katika mwili wa binadamu lakini watu wengi hupuuzia. Je, ushawahi kujiuliza ni kiasi gani maji yana umuhimu mwilini mwako? Kwa uhakika maji ni muhimu sana katika maji. 

Unaweza ukaishi kwa wiki kadhaa, lakini huwezi kuishi zaidi ya siku 5-7 bila maji. Maji mwilini mwako yakipungua kwa asilimia 1 tu, utasikia kiu. Na yakipungua zaidi ya asilimia 5,misuli huishiwa nguvu, uchovu na hujisikia umechoka. 

 Maji yakipungua zaidi ya asilimia 10, kizunguzungu na macho kutokuona vizuri hutokea. Ikifika asilimia 20 chini ya kiasi cha kawaida husababisha kifo.



Hamna kirutubisho muhimu katika mwili wa binadamu zaidi ya maji. Na hamna kirutubisho kingine ambacho kimechukua asilimia kubwa ya mwili wa binadamu zaidi ya maji. Mwili wa mwanaume una maji kiasi cha asilimia 60%, wa mwanamke una kiasi cha asilimia 50. Je wajua akili ya mwanadamu ina maji asilimia 75.
Tishu
Asilimia ya Maji
Damu
83.0
Moyo
79.2
Msuli
75.6
Ubongo
74.8
Ngozi
72.0
Mfupa
22.0
Kila siku tunapoteza robo 2 hadi 3 za maji kupitia haja ndogo, kutokwa jasho na kuhema. Ni muhimu kuongeza kiwango chako cha maji kwakua mifumo mingi ndani ya mwili wako hutegemea uwepo wa maji tosha.



No comments:

Post a Comment