FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI KWA
MAMA MJAMZITO
mwanamke mjamzito akifanya mazoezi |
Madaktari na wataalamu wa afya duniani
wanashauri mama mjamzito kufanya mazoezi mepesi kila siku kwa muda wa dakika 10
mpaka 30 kuimarisha mwili, mzunguko wa damu, viungo vya uzazi, kupunguza uzito
pamoja kuimarisha kinga za mwili zinazopambana na magonjwa.
Faida atakazopata
mama mjamzito endapo atafanya mazoezi.
1. Mazoezi huongeza nguvu za mwili.
1. Mazoezi huongeza nguvu za mwili.
3. Mazoezi hukufanya ujisikie vizuri na kukufanya uwe katika hali ya furaha.
4. Mazoezi hufanya mwili wako urudi upesi katika muonekano wake wa kawaida baada ya kujifungua.
5. Mazoezi husaidia huongeza mtiririko wa damu na hewa katika ngozi na kuifanya ngozi yako ionekane nzuri.
6. Mazoezi hupunguza maumivu ya
mgongo na huimarisha mifupa ya mgongo, makalio na mapaja na kuifanya iwe na
uwezo wa kuvumulia vyema uzito wa motto aliye tumboni
7. Mazoezi humsaidia mama mjamzito
apate usingizi kwa wepesi na kulala vyema.
8. Mazoezi hutayarisha mwili wako uwe tayari kwa ajili ya kuhisi uchungu kwa muda mfupi na kujifungua kwa urahisi.
9.mazoezi husaidia kuondoa usingizi na maumivu ya viungo
10. Mazoezi hupunguza maumivu ya
kichwa, kukosa choo na kuvimba mwili.
No comments:
Post a Comment