Malaria ni ugonjwa wa kuambukiza unaobebwa na vekta na kusababishwa na
kijiumbe ekaryoti protist aina ya plasimodium.
Mara nyingi huitwa "homa", ingawa homa
ni dalili mojawapo tu pia kuna magonjwa mengi yanayosababisha homa. Malaria
imeenea katika maeneo ya kitropiki hasa maeneo ya Amerika, Afrika, Asia.
Kila mwaka, kuna takriban
maambukizi milioni 350-500 ya malaria, kati ya watu milioni moja na tatu hufa, wengi
wao .Asilimia tisini ya vifo
vinavyosababishwa na malaria hutokea katika mataifa ya kusini mwa Afrika.
wakiwa watoto wachanga katika mataifa ya Afrika kusini mwa jangwa la
Malaria ni mojawapo ya magonjwa ya kuambikiza yaliyoenea sana na ni tatizo
kuu la afya ya
umma.
Kawaida, watu hupata ugonjwa wa malaria kwa kung'atwa na mbu wa kike wa jamii ya Anopheles
aliyeambukizwa.
Mbu aina ya Anopheles pekee ndio wanaoweza kusambaza
malaria, na ni lazima wawe wameambukizwa kupitia damu waliyofyonza kutoka kwa
mtu aliyeambukizwa. Mbu akimng'ata mtu aliyeambukizwa, kiasi kidogo cha damu
huchukuliwa, damu hiyo huwa na vimelea vya malaria.
Wiki moja baadaye, wakati
mbu anapofyonza mlo wake mwingine wa damu, vimelea hivyo huchanganyika na mate
ya mbu na kuingia katika mfumo wa damu ya anayeng'atwa. Vimelea hivyo huzaa
ndani ya seli nyekundu za damu,na kupelekea mgonjwa kupata ,homa, baridi, kichefuchefu, ugonjwa kama mafua,kukosa hamu ya kula na katika hali mbaya zaidi kupoteza
fahamu na hata kifo.
Maambukizi ya malaria yanaweza kupunguzwa kwa kuzuia
kung'atwa na mbu, kutumia vyandarua
vya vilivyo na dawa,kuziba mifereji na kuondoa maji yaliyosimama
ambapo mbu hutaga mayai yao, kuvyeka vichaka.
Watalaamu wa afya wanashauri kila uonapo moja ya dalili za Malaria unashauriwa kuwahi Hospitali ili kupata tiba ya haraka na sahihi na kwa wakati.
No comments:
Post a Comment