Monday 22 September 2014

UBOVU WA MIUNDOMBINU NA VITA VYA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO



mama mjamzito akipelekwa hospitali






















































































UBOVU WA MIUNDOMBINU NA VITA YA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO
Juhudi za kudhibiti na kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga zinaelezwa kuwa bado ni vitendawili katika maeneo mbalimbali.

Hali hii inaashiria Tanzania ipo katika wakati mgumu kutekeleza mpango wa malengo maendeleo ya millennia [MDG] ambao utafika kikomo mwakani 2015.
Sababu za ugumu huo unachangiwa na ubovu wa miundombinu ya barabara, uhaba wa wahudumu wa afya, na vitendea kazi.

Inaelezwa kuwa maeneo maeneo ya vijijini ndiko tatizo kubwa linapoanzia, ambapo miundombinu ya 
barabra limekuwa kikwazo, huku wajawazito wanapakiwa katika baiskeli, pikipiki, na machela kwa umbali mrefu kufikia kituo cha afya.

Hali hiyo ya ubovu wa miundombinu unachangia kuongezeka kwa vifo vya watoto wachanga na mama wajawazito.

No comments:

Post a Comment