Tuesday 23 September 2014

UELEWE UGONJWA WA EBOLA



UELEWE UGONJWA WA EBOLA

 muunekano wa kirusi cha ebola
JE! Zipi dalili za kwanza ambazo mtu anaweza kugundua kwamba ameambukizwa ugonjwa wa ebola ?

 muunekano baada ya kupata maambukizi ya EBOLA
Maradhi haya  ya ebola yanaenezwa na virusi. Dalili muhimu ni kwamba mtu anaweza kutokwa na damu katika sehemu za wazi za mwili kama puani, mdomoni, masikioni, njia ya aja ndogo na kubwa.

Lakini kabla ya kufika katika daraja hili la kutokwa na damu sejhemu wazi, kwanza  mtu anaweza kupatwa na homa kali, kutapika, kuharisha, kukosa hamu ya kula, na kuwa dhaifu [mnyonge],  maumivu ya viungo vya mwil, kuumwa tumbo na kichwa

HUDUMA YA KWANZA
 Mgonjwa wa EBOLA

Kwanza kabisa ni muhimu kuwahi kufika kituo cha tiba [afya] haraka iwezekanavyo. Kuvigundua virusi vya ebola kuna hitaji utaalamu wa hari ya juu wa maabara.

Jambo la kwanza ni kuchunguza na kuhakiki kwamba ni kweli mtu ameambukizwa virusi vya ebola.
Pili, kumtenga na watu wengine ili yeye nwenyewe asidhurike zaidi na asiwadhuru wengine.

UNAWEZAJE KUPATA EBOLA

Kwa bahati nzuri virusi vya ebola hazienezwi kwa njia ya hewa air [born]. Ebola inaenezwa kwa mtu kugusna na majimaji ya mwili kama vile damu, machozi, jasho, manii.


Waatalamu wa afya wanasema njia bora ya kujikinga na ebola ni kuongeza usafi wa mwili na mazingira pamoja na kujenga mazoea ya kunawa mikono kila wakati ielewe ebola

No comments:

Post a Comment